Headlines

Kuna kusudi

Sio kila Mtu anayeondoka kwenye Maisha YAKO ni HASARA:-
.
1) Kuna wengine inawabidi waondoke ili uanze kujitambua na kujiamini katika maisha. Kuna watu unaweza kujikuta unawategemea sana hadi unapoteza uwezo wako wa kusimama mwenyewe.
.
2) Kuna wengine wanaondoka ili watengeneze nafasi ya watu wengine unaowahitaji kwa wakati huo waje. Kuna watu ukiendelea kukaa nao ni kizuizi kwa wengine kuja kwenye Maisha Yako.
.
3) Kuna ambao wanaondoka kwa sababu Muda wao na jukumu lililowaleta kwenye MAISHA YAKO limeshaisha. Watu wa namna hii ukiendelea kuwalazimisha kubakia mtakuja kuachana kwa magomvi mengi sana na mtachukiana baada ya hapo.
.
4) Kuna wengine wanaondoka ili wakusaidie uanze kufanya maamuzi sahihi ambayo umekuwa unaghairisha kwa sababu ya kuwaogopa ama kwa sababu ushawishi wao umekupelekea kufanya wanachokiamini wao na sio kile unachokiamini wewe. .
.
Jifunze kutowang’ang’ania watu kwenye Maisha yako muda wao wa kuondoka unapofika.Sio kila anayeondoka ni hasara kwako,kuna wengine kuondoka kwao ni faida kubwa kwako. . .
.kujitambua na kujiamini katika maisha. Kuna watu unaweza kujikuta unawategemea sana hadi unapoteza uwezo wako wa kusimama mwenyewe.
.
2) Kuna wengine wanaondoka ili watengeneze nafasi ya watu wengine unaowahitaji kwa wakati huo waje. Kuna watu ukiendelea kukaa nao ni kizuizi kwa wengine kuja kwenye Maisha Yako.
.
3) Kuna ambao wanaondoka kwa sababu Muda wao na jukumu lililowaleta kwenye MAISHA YAKO limeshaisha. Watu wa namna hii ukiendelea kuwalazimisha kubakia mtakuja kuachana kwa magomvi mengi sana na mtachukiana baada ya hapo.
.
4) Kuna wengine wanaondoka ili wakusaidie uanze kufanya maamuzi sahihi ambayo umekuwa unaghairisha kwa sababu ya kuwaogopa ama kwa sababu ushawishi wao umekupelekea kufanya wanachokiamini wao na sio kile unachokiamini wewe. .
.
Jifunze kutowang’ang’ania watu kwenye Maisha yako muda wao wa kuondoka unapofika.Sio kila anayeondoka ni hasara kwako,kuna wengine kuondoka kwao ni faida kubwa kwako.
Nukta

Share this:

1 comment :

 
Copyright © Yote Yanawezekana Kwa Yesu. Designed by OddThemes