Headlines

YOTE YANAWEZEKANA

Yesu akawakazia macho, akasema, Kwa wanadamu haiwezekani, bali kwa Mungu sivyo; maana yote yawezekana kwa Mungu.

Marko 10:27
Ni wazi kua hakuna jambo lolote lililo gumu la kumshinda Mungu.
Watu wengi wamekua wakikosa kutendewa miujiza kwa sababu tu wamekosa kumwamini Mungu kua anazo nguvu za kuwaokoa katika misiba waliyo mayo.
Ngoja nikufundishe kidogo imani ni nini?
Ni kua na uhakika kabisa,kwa asilimia zote.

Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Waebrania 11:1

Unapo kosa kua na imani amefunga mlango wa kumruhusu Mungu ,kutenda jambo kwako.

Mungu anataka moyo wako.kitu unacho kiamini ni kwamba kitu hicho umekipa moyo wako.

Na kukipa kitu Moyo ni kuanza kukitegemea hicho.
Ndio maana Mungu akawa mkali akisema  amelaaniwa mtu yule amtegemeaye Mwanadamu.

Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.

 Yeremia 17:5
Yesu aliponya watu kwa kua walikua na imani.Hata alipo kwisha kuwaponya alisema  Imani yako imekuponya.
Imani inamruhusu Mungu kukufanyia jambo.

Imani yako ukiiweka kwa Mungu ni wazi hakuna litakalo shindikana .

Ndio maana neno linasema

Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
Marko 9:23
Ukiwa na imani Nguvu ya Mungu inafanya kazi ndani yako.
Wanafunzi wa Yesu walikua wakipitishwa na Yesu katika fundisho la imani, kama funguo ya kufanya mambo ambayo wengine wasije weza kufanya.

Wanafunzi wa Yesu walipo kosea mahesabu Yesu alikasirika
Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

Mathayo 17:19-20
Kitu ambacho kili fanya wanafunzi wa Yesu kushindwa kumtoa pepo ni? Upungufu wa imani zao.

Kitu kinacho kufanya uendelee kukaa katika hali uliyo nayo ni upungufu wa imani.
Usipo weka imani kwa Mungu mambo mengine hayata wezekana kwako.
Weka imani kwa  Mungu, hakuna litakalo shindikana kwako.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © Yote Yanawezekana Kwa Yesu. Designed by OddThemes